2. MALEZI YA MTOTO KATIKA UMRI WA UTOTO

Utoto

Kipindi hiki huanza mwezi wa kwanza mpaka mtoto anapofikisha mwaka mmoja. Ukuaji na maendeleo ya mtoto katika kipindi hiki huwa ni haraka

Maendeleo ya mwili

Maendeleo ya mwili wa mtoto ni uwezo wa mtoto kutumia na kudhibiti mwili wake. Maendeleo ya kimwili yaendane na ukuaji wa mtoto na kukua kwa ujuzi wa mwili ikiwa ni pamoja na akili, misuli na akili. Mfano ; Watoto hujifunza dunia yao wanapo ona, shika, kunusa, kusikia na ladha

Hatua kuu za utotoa

  • Anashikila kichwa thabiti
  • Anarefuka
  • Anakaa chini
  • Anatambaa
  • Anasimama mwenyewe
  • Anatembea mwenyewe

Kichochea maendeleo ya mwili wa mtoto

Wazazi ili kusaidia maendeleo mazuri ya mwili wa mtoto, tumsaidie mtoto kwa kushikilia mwili na kichwa tunapowashika. Tuwasaidie watoto kuona sura zetu tunapoongea na kucheza nao. Tuwape nafasi ya kujifunza na kutumia ujuzi kama kukaa chini huku akimsaidia shingo yake na mgongo. Wazazi waeke vitu karibu na kuwapa nafasi watoto ya kufikia vitu. Watoto watengenezewe mazingira salama kwaajili ya kutambaa na kujifunza vitu mbalimbali. Wazazi wampe mtoto vitu vya kuchezea vitakavyomsaidia mtoto katika maendeleo ya mwili wake

Watoto huzaliwa na matendo yasiyo ya hiyari, matendo hayo hufurahisha watoto wanapoyafanya. Wanapokuwa wakubwa matendo hayo hupotea

  1. Mtoto anafungua mdomo kwaajili ya kunyonya wanapohisi Kuna kitu karibu ya mdomo
  2. Mtoto anaposhika kitu vizuri kwa mkono wake
  3. Mtoto anatupa miguu, mikono na kichwa huku analia
  4. Mtoto anapojikunja mwili wake anaposhika kwa vidole mgongoni au miguuni

Uwepo wa vitendo hivi kwa mtoto ni muhimu sana, ni ishara ya maendeleo ya mfumo wa neva kufanya kazi vizuri

Dalili/Ishara kuharibika maendeleo ya mwili wa mtoto

  1. Mtoto hawezi kutupa mikono
  2. Mtoto hawezi kusimamisha shingo
  3. Mtoto anamiguu na mikono migumu/dhaifu
  4. Mtoto hawezi kukaa chini au kutambaa
  5. Mtoto hawezi kujilisha mwenyewe

Maendeleo ya utambuzi ( Utoto)

Katika hatua ya utoto mtoto hutumia akili, ukuaji wa mwili na uwezo wa kushika vitu humsaidia mtoto kujitofautisha na vitu

Uwezo wa utambuzi (Utoto)

Vitendo mtoto anatakiwa afanye kuonyesha anauwezo wa utambuzi (mtoto akiwa na miezi 6)

  • Mtoto anatambua sura anazozifahamu na kujua sura ambazo hazifahamu
  • Mtoto anapenda kucheza na wengine, hasa wazazi
  • Mtoto hujibu hisia za wengine na kufurahia
  • Mtoto anapenda kujiangalia mwenyewe katika kioo

Mzazi mzuri

Mzazi mzuri humsaidia mtoto katika ukuaji wake kwa kufanya yafuatayo;

  • Muoneshe/fanya unachotaka mtoto akifanye
  • Muhimize mtoto acheze
  • Muhimize mtoto katika kutatua matatizo
  • Mfundishe mtoto mipaka
  • Msaidie mtoto kujua hisia zake na za watu wengine

Usisahau kurudi tena kwaajili ya hatua nyingine za ukuaji wa mtoto!

Leave a comment

Design a site like this with WordPress.com
Get started