MALEZI YA MTOTO NA UKUAJI WA MTOTO

Ukuaji wa mtoto

Hatua za ukuaji wa mtoto

Ukuaji wa mtoto umegawanyika katika hatua sita, kila hatua huleta uwezo na matarajio mapya katika jamii na kutumika kama mapito muhimu katika ukuaji wa mtoto


1. Kabla ya kujifungua

Kabla ya kujifungua

Chembe moja kiumbe hubadilishwa na kuwa mtoto mwenye ajabu ya uwezo wa kujibadilisha kwenda kwenye maisha katika mazingira ya duniani

Hatua kabla ya kujifungua

Kipindi cha kuota

Hiki ni kipindi kati ya utotoleshaji mpaka upandikizaji wa mtoto. Kipindi hiki huchukua takribani siku 14

Kipindi cha kiinitete

Hiki ni kipindi kati ya upandikizaji mpaka kiinitete kimetengeza viungo vikuu vya mtoo. Kipindi hiki huchukua takribani miezi 3. Katika kipindi hiki mtoto viungo vyake muhimu hujitengeneza, huonyesha utofauti wa kijinsia na mtoto huanza kujibu kichocheo cha moja kwa moja

Kipindi cha fetasi

Kipindi hiki kuanza mara tu mifupa ya mtoto inapoanza kuwa migumu. Huanza takribani miezi 3 mpaka mtoto anapozaliwa

Kabla ya kujifungua kipindi cha kiinitete ni kipindi muhimu sana. Ukuaji wa fetasi katika tumbo huwa wa haraka katika kipindi cha kiinitete. Hali isiyo ya kawaida katika viungo vya mtoto inaweza tokea. Tuwe makini sana na kuzingatia katika kipindi hiki ili kumlinda mtoto

Ukuaji wa akili ya mtoto

Ukuaji wa akili wa mtoto huanza ndani ya siku 30, ifikiapo siku ya 40 adi 100 saizi ya ubongo huongezeka. Ifikipo miezi mitano sehemu muhimu za akili ya mtoto huanza kukua. Miezi tisa akili ya mtoto inakuwa tayari kwaajili ya mtoto kuweza kuzaliwa

Maendeleo ya uwezo wa utambuzi

Wakati mtoto yupo tumboni huanza kujifunza lugha kutoka kwa mama ake. Mtoto akiwa tumboni husikiliza mazungumzo ya mama ake katika wiki 10 za mwisho za ujauzito na wakati wa kuzaliwa huenda akaonyesha alichokisikia

Maendeleo ya uwezo wa kihemko wa kijamii

(Afya ya mama mjamzito na mtoto)

Ulinzi wa mtoto huanza kwa kumlinda mama anayetarajia kujifungua mtoto. Utafiti unaonyesha mama wajawazito wenye msongo wa mawazo na unyanyasaji wa kimwili hujifungua watoto wachanga wenye kasoro

Mama mjamzito apate msaada wa familia. Uwepo wa mwenza mwenye huruma na watu wengine wenye msaada katika familia,kazi chache za nyumbani na ajira dhabiti

Mama mjamzito hatakiwi kuwa na msongo wa mawazo, hupelekea mama mjamzito kujifungua mtoto mwenye uzito mdogo sana

Pombe kwa mama mjamzito ni hatari, mama mjamzito atumiapo pombe hupelekea madhara kwa mtoto. Mtoto anaweza kupata kichwa kidogo kisichokuwa cha kawaida, ukuaji mdogo wa akili ya mtoto,magonjwa ya moyo na matatizo ya viungo

Swali: Kwanini wanawake wanatoa mimba? Tufanye nini kuzuia utoaji wa mimba?

Leave a comment

Design a site like this with WordPress.com
Get started