4. MALEZI YA MTOTO KATIKA UMRI WA UTOTO WA MAPEMA

Utoto wa mapema

Utoto wa mapema ni kipindi kati ya miaka 4 adi 7. Ni kipindi ambacho mtoto hupata elimu yake ya awali ( chekechea)

Ukuaji wa mwili

Mtoto katika kipindi hiki huongezeka takribani kilo 1.8 kila mwaka na urefu wa mtoto huongezeka

Muonekano wa mwili

Mtoto huwa mrefu na mwili hupungua ukilinganisha na mtoto mdogo. Miguu yake na sehemu nyingine za mwili huendelea kukua, kichwa chake huwa kidogo ukilinganisha na mwili wake

Harakati na vitendo vya misuli

Harakati na vitendo vya misuli katika kipindi hiki ni matokeo ya maendeleo ya mwili wa mtoto. Mtoto mwili unavyoendelea kukomaa pia huendelea kuimarisha misuli yake na uwezo wa kudhibiti mwili wake vizuri

Ujuzi katika maisha

Mtoto anakuwa katika harakati za kila wakati, harakati na vitendo vya misuli ni vya kusudi zaidi. Mtoto hutumia muda mwingi katika shughuli za mwili kama vile kukimbia, kupanda vitu mbalimbali, kuruka na kukimbia

Hatua kuu za utoto wa mapema

  • Aweze kutumia uma na kijiko
  • Aweze kubembea na kuponda vitu
  • Aweze kuruka vitu

Kusisimua kwa mwili (Utoto wa mapema)

Mzazi mruhusu mtoto acheze lakini katika mazingira yaliyo salama kwa mtoto. Tumuangalie mtoto anapokuwa anacheza na uhakikishe unajumuika katika michezo yake. Muache mtoto azunguke na achunguze ili akuze maendeleo ya hisia. Walimu wahakikishe kwamba darasa linahusisha harakati za mwili

Kujifunza kwa mtoto ( Utoto wa mapema)

Mtoto katika kipindi hiki hujifunza kwa kupitia kugundua, kuchunguza, majaribio na kutatua matatizo

Uwezo wa utambuzi

Mtoto wa shule ya awali huanza kuona vitu kutokana na mtazamo wa watu wengine na huanza kuelewa jinsi tabia zao zinavyoathili watu wengine. Mtoto anaendeleza ujuzi wake wa lugha ya mdomo, kupata misamiati mipya na muundo wa sentesi. Mtoto anaelewa dhana ya nafasi,mda na vipimo lakini pia dhana kama jana, leo na kesho. Mtoto anajua kushoto na kulia. Mtoto huanza kukuza hali ya kujiamini na uwezo wa kujifunza. Mtoto hujifunza kusema na kuandika na anauwezo wa kutamka maneno rahisi. Mtoto anaanza kujadili na kubishana, anauwezo wa kufanya hesabu rahisi

Kusisimua utambuzi (Utoto wa mapema)

Tuwe mfano kwa mtoto, mtoto hufanya yale wanayotuona tunafanya. Mtoto aulizwe maswali ya wazi anayoweza kuelewa. Mtoto apatiwe vifaa kumtia moyo kutatua matatizo na ugunduzi

Maendeleo ya kihemko ya kijamii

Maendeleo ya kihemko ya kijamii katika hiki kipindi inahusisha mtoto kujitegemea katika vitu kama mazoea, kushilikiana na wenzake, kujua maana ya uhusiano na watu wengine, kudhibiti hisia na kukuza muonekano wake binafsi. Saikolojia inasema mtoto katika hiki kipindi humpenda zaidi mzazi wa jinsia tofauti tofauti na yake, kumsaidia mtoto kufafanua jinsia yake. Mtoto hupata upendo wake wa kwanza na jinsi ya kushughulikia mapenzi kwa kina

Hatua za kihemko za kijamii

Mtoto hukuza uelewa wa huruma, kutengeneza na kutunza mahusiano mazuri na urafiki. Mtoto anaanza kukuza hali ya maadili lakini pia kutambua na kusimamia hisia zake. Mtoto hutengeneza mtazamo chana wa kujitambua yeye mwenyewe na maoni kuhusiana na maadili na kujifunza baya na zuri, mtoto anakuwa na uwezo wa kuonyesha mtazamo wake na majadiliano ya mtazamo wake. Mtoto anaanza kuelewa mambo mbalimbali yanayo mzunguka na hata kuigiza maswali kuhusu kifo. Mtoto hukubali kwamba wazazi sio watu wenye nguvu mda wote. Mtoto atataka kuwaomba msamaha marafiki zake, kukubali na sheria zinazowekwa, kupenda kuimba , kucheza mziki na kuigiza, kujua maana ya jinsia yake na kuweza kusema lipi ni la kweli pamoja na vitu vinavyoweza kukuaminisha

Umuhimu wa hatua za kihemko za kijamii

Hatua za kihemko za kijamii ni za muhimu sana kwa mafanikio ya mtoto shuleni na nyumbani na ukuaji wa mtoto kwani ujumla

Matatizo ya kihemko ya kijamii

  • Kushindwa shule
  • Kukosa marafiki
  • Kujitenga na jamii
  • Kuwa na aibu
  • Kutaka kuwa na nguvu

Mzazi muwajibikaji

Mzazi muwajibikaji katika kipindi hiki hutatua matatizo ya mtoto na kumsaidia kuongelea hisia zao pamoja na wenzao. Mzazi kumuelewa mtoto na kumsaidia kuwa karibu na mzazi wa jinsia nyingine lakini pia ni mda mda wa kuwaelekeza katika maadili mazuri. Mzazi amsaidie mtoto mtoto kuweza kuzuia hisia za zake na kujua umuhimu wa kuanzisha mipaka (heshima). Mzazi amruhusu mtoto kucheza na watoto wengine na kumpatia vitu vya kuchezea vitakavyokuwa msaada katika ukuaji. Mzazi acheze pamoja na watoto na kuangalia kwa ukaribu michezo wanayocheza. Mzazi afuate muongozo wa mtoto, ampe msaada vitu mtoto anaufahamu navyo na kujifunza

Malezi mabaya

  • Lugha ya matusi kwa mtoto
  • Upendeleo wa mtoto
  • Ubaguzi wa

Malezi ni malengo

ParentingTanzania

Leave a comment

Design a site like this with WordPress.com
Get started