MALEZI YA MTOTO NA UNYANYASAJI WA WATOTO

Unyanyasaji wa watoto

Unyanyasaji wa watoto ni vitendo vya unyanyasaji na kupuuzwa vinavyotokea kwa watoto chini ya miaka 18. Inahusisha vitendo vyote vya unyanyasaji wa kimwili, kihisia, kijinsia, kupuuzwa, uzembe, kibiashara na unyonyaji mwingine ambayo hupelekea uhalisia wa madhara kwa afya za watoto, kuishi heshima, mahusiano majukumu, majukumu, uaminifu na nguvu

Ukubwa Wa Tatizo La Unyanyasaji Wa Watoto

Unyanyasaji wa watoto ni tatizo la duniani kote na huleta athari mbaya katika maisha. Japokuwa tafiti nyingi zimefanywa bado nchi nyingi hazina idadi kamilifu ya vitendo vya unyanyasaji wa watoto. Unyanyasaji wa watoto ni ngumu sana kufanyia utafiti, kwa sababu kila nchi ina namna yake ya kufanya utafiti kutegemea na

  • Maana ya unyanyasaji wa watoto inavyotumika
  • Aina ya unyanyasaji wa watoto inavyofanyiwa utafiti
  • Ubora wa takwimu
  • Ubora wa utafiti

Bila kikomo tafiti nyingi zimeonyesha kwamba karibia watoto wa 3 katika watoto wa 4 kati ya miaka 2 mpaka 4 hupata adhabu za kimwili au mvurugo wa kisaikolojia katika mikono ya wazazi au walezi na imeripotiwa kati ya wanawake 15/13 wanaume mmoja alipata manyanyaso ya kijinsia wakati wa utotoni

Kila mwaka, inakadiriwa katika kifo cha mauaji kwa watoto chini ya miaka 18 hutokana na unyanyasaji wa watoto

Matokeo Ya Unyanyasaji Wa Watoto

Unyanyasaji wa watoto husababisha mateso kwa mtoto na familia na inaweza kuwa na athari mbaya katika maisha. Unyanyasaji wa watoto husababisha msongo wa mawazo inayohusishwa na uharibifu was ukuaji wa akili katika umri mdogo. Msongo wa mawazo uliozidi inaweza kudhoofisha ukuaji wa mfumo wa neva na kinga. Watu wazima waliopata unyanyasaji utotoni wako katika hatari zaidi ya tabia, mwili na matatizo ya afya ya akili kama:

  • Huzuni
  • Kuvuta sigara
  • Unene kupita kiasi
  • Tabia hatari za ngono
  • Ujauzito usiokusudiwa
  • Pombe na matumizi ya dawa za kulevya
  • Magonjwa ya moyo
  • Kansa
  • Kujiua
  • Maambukizi ya zinaa

Ukatili dhidi ya watoto ni sababu moja wapo inayopelekea kutokuwa na usawa katika elimu, zaidi ya matatizo ya afya, jamii na elimu kuna athari za kiuchumi kama: matibabu ya kiafya

Sababu Za Athari

1. Wazazi/Walezi

Ni muhimu sana kusisitiza kwamba watoto ni wahanga na haipaswi kuwabebesha lawama za unyanyasaji wa watoto

Sifa za mtoto ambaye anaweza kupata manyanyaso

  • Mtoto kuwa chini ya miaka 4 au balehe
  • Mtoto kushindwa kutimiza matarajio ya mzazi
  • Mtoto mwenye mahitaji maalum, anayelia sana au kuwa na kasoro za kimwili
  • Kumuona mtoto yupo sawa na jinsia ya tofauti na yake au kuwa na jinsia mbili

Sifa za mzazi/mlezi ambaye anaweza kuongeza uwezekano was mtoto kufanyiwa unyanyasaji

  • Mzazi/mlezi hawezi kutengeneza mahusiano mazuri na mtoto
  • Mzazi/mlezi aliyepitia manyanyaso utotoni
  • Mzazi/mlezi hana uelewa na ukuaji wa mtoto
  • Mzazi/mlezi kutumia pombe kupita kiasi na matumizi ya dawa za kulevya
  • Mzazi/mlezi asiyeweza kujizuia hasira
  • Mzazi/mlezi mwenye matatizo ya akili
  • Mzazi/mlezi anayejihusisha na vitendo vya uhalifu
  • Mzazi/mlezi mwenye matatizo ya kifedha

2. Mahusiano

Tabia za mahusiano katika familia, marafiki na watu mbalimbali tunaoingiliana nao katika maisha inaweza kuongeza uwezekano wa mtoto kupata unyanyasaji

  • Kuvunjika kwa familia
  • Kutengwa katika jamii
  • Kuvunja usaidizi wa ndugu na jamaa katika malezi ya mtoto

3. Jamii

Sifa za jamii zinazoweza kuongeza hatari ya unyanyasaji wa mtoto ni pamoja na:

  • Usawa wa kijinsia wa jamii husika
  • Ukosefu wa nyumba za kutosha
  • Kiwango cha juu cha ukosefu wa ajira na umaskini
  • Upatikanaji rahisi wa pombe na dawa za kulevya
  • Sera na mipango isiyotosheleza kuzuia unyanyasaji wa watoto, upigaji picha za watoto,ukahaba wa watoto na ajira ya watoto
  • Kanuni za kijamii na kitamaduni zinazokuza unyanyasaji wa watoto
  • Sera za jamii, kiuchumi, kiafya na elimu zinazopelekea maisha duni

Kuzuia unyanyasaji wa watoto

Kuzuia na kuwajibika katika unyanyasaji wa watoto inahitaji mbinu ya kitabaka( ushirikiano wa wa wadau). Uingiliaji huo wa mapema hufanyika katika maisha ya watoto, huleta faida kubwa kwa mtoto na jamii

Uingiliaji mzuri na wa kuahidi ni pamoja na:

  • Usaidizi wa wazazi na walezi
  • Mbinu ya elimu na stadi za maisha
  • Kanuni na njia za kuthamini
  • Utekelezaji na uimarishaji wa sheria
  • Majibu na huduma za msaada
Tuache Unyanyasaji Wa Watoto
TUACHE

Leave a comment

Design a site like this with WordPress.com
Get started