Kila familia, shule na jamii kwa ujumla inawajibu ya kuwapa watoto ULINZI na kuhakikisha wako SALAMA. Ukiwa kama mzazi unawajibuwa kumlinda mtoto na kumsikiliza lakini pia kumfundisha kujilinda yeye mwenyewe.
NAMNA YA KUONGEA NA WATOTO KUHUSU ULINZI NA USALAMA WAO
Mzazi anawajibu wa kumfundisha mtoto kuhusu usalama wake yeye mwenyewe. Mzazi umfundishe ujuzi WA usalama kama vile kutumia akili kufikiria, kuwa na tabia ya kujiamini hasa hisia zake na kushirikiana na watu wengine. Hakuna umri sahihi wa mzazi kumfundisha mtoto usalama wake mwenyew anza sasa.
Mzazi msikilize mtoto wako ujue mambo yaliyokea katika siku yake mzima na tabia zake. Msikilize mtoto nini anapenda nini hakipendi. Mfanye mtoto ajue kwamba anaweza kuongea na wewe jambo lolote. Muhakikishie mtoto wako kwako ndio sehemu salama linapotokea tatizo lolote.
MAMBO YAKUMFUNDISHA MTOTO YATAKAYO MSADIA USALAMA WAKE
Mwambie mtoto atambue mipaka sehemu za kwenda wanachoweza kuona na vitu vya kufanya likitokea tatizo lolote. Mfundishe kujenga ujamaa asijitenge peke ake sehemu hatarishi lakini pia ni sawa kusema hapana kama anaona kuna jambo halipo sawa.
JUKUMU LA MZAZI KUHAKIKISHA USALAMA WA MTOTO
1. Lazima ujue mahali mtoto wako yupo mda wote
2. Mtoto akupe taarifa kama kuna tatizo lolote limetokea
3. Hakuna mtu mwingine anauepaswa kuwa makini na msimamia mtoto isipokuwa mzazi mwenyewe
USALAMA WA MTOTO NYUMBANI
1. Mtoto anatakiwa ajue jina lake lote namba ya simu ya wazazi, nyumbani ata ya mwanafamilia wa karibu
2. Kama mzazi haupo kuwa na mtu mzima anayeaminika ambaye mtoto anaweza kumpa taarifa anapopata tatizo
3. Chagua dada wa kazi kwa uangalifu mkubwa, baada ya kumpata dada wa kazi muulize mtoto wako maoni yake kuhusu dada wa kazi na usikilizekwa makini
4. Akague nyumba kwa nje kabla hajaingia, afunge milango, aite kujua kama kuna watu ndani, asiwape taarifa watu nyumbani yupo mwenyewe na asifungue mlango kwa mtu asiyemjua
USALAMA SHULENI
Mzazi kuwa makini na alama unazioekq kwenye vifaa vya shule vya mtoto vinaweza kuhatarisha maisha yake . Kuhakikisha usalama wa mtoto anapoenda na kurudi SHULENI. Jambo la msingi zaidi mtoto wako anapaswa kukwambia mambo yote yaliyotokea shuleni kwake siku mzima.
MAMBO MUHIMU MTOTO ANAPASWA KUYAFAHAMU
1. Jina lake
2. Majina ya wazazi
3. Mahali anapoishi
4. Namba ya simu ya mzazi
5. Kumpa taarifa mzazi kabla hajaend sehemu yoyote au mtu yoyote
6. Kumpa taarifa mzazi au mtu mzima anayeaminika kabla hajapokea chochote ata kutoka kwa mtu unayemfahamu
7. Acheze na marafik zake asicheze peke ake
8. Ni sawa kusema hapana kama anaona kuna jambo sio sawa, halielewi , linamnyima raha, linamkosesha amani au amekatazwa
9. Lazima amamwambie mzazi au mtu mzima anayeaminika anapopatwa na tatizo lolote
10. Ana haki ya kuwa salama
ULINZI NA USALAMA WA MTOTO NI JUKUMU LA KILA MMOJA WETU NA JAMII KWA UJUMLA
TUWALILINDE WATOTO WETU