Kila mtoto ni zawadi kutoka kwa Mungu. Furaha ya mtoto ni Jambo la muhimu ambalo kila mzazi anatamani mtoto wake awe nayo.
Katika tafiti zilozofanywa katika nchi 67 duniani zenye tamaduni tofauti, imani tofauti na vipato tofauti, wazazi kitu walichotamani kutokana na maswali waliyoulizwa ni watoto wao kuwa na furaha.
Ni lazima kila mzazi aelewe huwez kufanya mtoto wako akawa na furaka, Ila unaweza kufanya mambo yatakayo mtia nguvu aweze kuitafuta furaha yake yeye mwenyewe. Jambo la kuzingatia wewe kama huwezi huwezi kufanya mtoto awe na furaha isipokuwa unaweza kumtia mtoto nguvu kuitafuta furaha yake ya kweli yeye mwenyewe.
Katika kumfanya mtoto awe na furaha mzazi anaweza kufanya nakosa ambayo yakapelekea mtoto asiwe na furaha kwa mzazi kuamini kwamba anajua kilicho Bora kwa mtoto wake.
Furaha ya kweli sio ile mtoto unayompatia bali ni ile atakayoitafuta mwenyewe baada ya mzazi kumsaidia kwa kumpa nguvu kuipata furaha yake ya kweli.
Msaada wa mzazi ni mwanzo mzuri wa kumuwezesha mtoto kuwa na furaha ya kweli. Tuwape msaada kutafuta furaha zao wenyewe tusiamini tunaweza kuwapa furaha. Kwa kuongezea furaha za watoto hutofautiana tuzingatie hilo sana.
Kila analofanya mzazi ni hamu ya kuona mtoto wake anafuraha, hivyo tuwasaidie watoto wetu kuitafuta furaha ya kweli wenyewe kwa kuwapenda. Tunavyowasaidia watoto kutafuta furaha ya kweli malipo yake mzazi atapata furaha pia.
MALEZI NI FURAHA, FURAHIA KUWA MZAZI
